Monday, June 19, 2017

USEMAVYO MKATABA WA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU

Kutokana na tukio la majuzi la kupigwa na kiteswa kwa watu wenye ulemavu nchini Tanzania wakidaiwa kufanya maandamo,  wakidai yako yao ya msingi iliyomo kwenye mkataba wa kimataifa IBARA YA 27 KIPENGERE CHA (f) “Kuendeleza ajira binafsi, fursa za biashara, ushirika na kuanzisha biashara;” na hii ni mahususi kwa watu wenye ulemavu pamoja ibara na vingere vingine vingi kama nilivyoviolozesha hapa chini.
Pia katika mkataba huu ni kwamba haujaacha kitu kwani umetowa majukumu mazuri na makubwa ya kutekerezwa kwa kila idara ya wizara na taasisi zote nini wajibu wao juu ya watu wenye ukemavu ikiwemo jeshi la police,  kinachonisikitisha ni kwamba elimu haijafika kwa wahusika hususani jeshi ka police nduo maana hawazinmtambuwa haki za wenye ulemavu kwa mjibu wa mkataba huu.
Mimi kama mwanaharakati natamani sana kila mtu atambuwe namna mkataba huu unavyosema ila nashindwa kuelewa mamlaka zinazohusika kwanini mpaka leo kuna watu au taasisi ambazo dhahili zimeonyesha kutombua na kufahamu mkataba huu unavyowataka kuwatendea watu wenye ulemavu,  na yote hii ni kwa sababu mamlaka zinazohusika zimeshindwa kuufikisha na kusambaza elimu hii mhimu iliyosainiwa na serikali yetu chini ya MHE: RAIS DK JAKAYA MRISHO KIKWETE.  Mwaka 2009.

IBARA NA VIPENGERE VYA
MKATABA WA KIMATAIFA WA HAKI ZA WATU WENYE UKEMAVU.

IBARA YA 1-- MADHUMUNI
Maafikiano haya yameandaliwa ili kuhakikisha kwamba:Watu wenye ulemavu ni pamoja na watu wenye vilema vya kudumu (mathalani: viungo, akili n.k) na wale ambao kwa sababu mbalimbali
hawajumuishwi katika jamii (mfano kutokana na vizuizi vya kimtazamo,
lugha, mazingira na sheria).

IBARA YA 11-- HALI YA HATALI NA DHARULA.
kutokana na majanga Nchi zitahakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanalindwa wakati wa vita, majanga ya asili au
dharura nyinginezo.

IBARA YA 15 -- KUTOFANYIWA MATESO UKATILI AU KUDHALILISHWA.
1. Hakuna mtu atakayeteswa, kutendewa au kuadhibiwa katika hali ya kikatili au
kiudhalilishaji. Hakuna mtu atakayelazimishwa kushiriki katika majaribio ya kisayansi au kitabibu.

IBARA YA 16 -- KUTINYONYWA KUTOFANYIWA VURUGU AU KUNYANYASWA.
Nchi:
1. Zitapitisha sheria na kuchukua hatua
nyinginezo ili kuhakikisha kuwa watu wenye
ulemavu hawanyonywi au kudhalilishwa
wakiwa nyumbani au nje ya nyumbani.
2. Zitachukua hatua ya kuzuia udhalilishaji wa watu wenye ulemavu kwa kuwapa misaada na taarifa sahihi wao wenyewe
na familia zao.
3. Zitahakikisha kuwa sehemu na programu zinazowa-hudumia watu wenye ulemavu zinakaguliwa kila mara ili kudhibiti ukatili na manyanyaso

2. Nchi zinakubaliana,  kutunga sheria na kuchukua hatua nyingine ili kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu
wanalindwa dhidi ya mateso kama ilivyo kwa watu wengine.

IBARA YA 27 - KAZI NA AJIRA.
1. Watu wenye ulemavu wana haki ya kufanya kazi sawa na watu wengine;
wana haki ya kupata riziki kutokana na
kazi walizojiamulia kuzifanya katika
mazingira yaliyo wazi na yanayofikiwa na watu wote. Nchi zitatunga sheria na kuchukua hatua nyingi zinazofaa ili:
a) Kuondoa ubaguzi kwa misingi ya ulemavu katika maeneo yote ya ajira ikiwa ni
pamoja na katika hali ya kutafuta kazi, kuajiriwa kuendelea na ajira, kupandishwa cheo
kazini na kufanya kazi katika mazingira salama kiafya;
b) Kulinda ajira za watu wenye ulemavu kuhusu usawa katika malipo ya ujira kwa kazi
ile ile, usawa wa fursa, usalama kazini na uwezo wa kutoa malalamiko;
c) Kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanaweza kujiunga pamoja na kuingia
kwenye vyama vya wafanyakazi sawa na mtu mwingine yeyote;
d) Kuweka uwezekano wa watu wenye ulemavu kupata huduma za ushauri wa
mafunzo kazini.
e) Kupanua fursa za kazi, kuandishwa vyeo na kuwasaidia watu wenye ulemavu
kutafuta kazi na kudumu kazini;
f) Kuendeleza ajira binafsi, fursa za biashara, ushirika na kuanzisha biashara;
g) Kuajiri watu wenye ulemavu serikalini;
h) Kuhimiza na kuwasaidia waajiri kuajiri watu wenye ulemavu;
i) Kuwarahisishia watu wenye ulemavu kumudu kazi na mazingira yake kwa
kuhakikisha kuwa marekebisho yanafanyika kwa ajili yao;
j) Kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanapata uzoefu wa kazi katika soko la ajira;
k) Kukuza programu zinazowasaidia watu wenye ulemavu kurudi kazini na kudumu na
ajira zao.
2. Nchi zitahakikisha kuwa watu wenye ulemavu hawafanywi watumwa/watwana. Nchi zitawalinda dhidi ya ajira za kushurutishwa sawa na wanavyolindwa watu wengine.

Mwisho naomba nisisitize kuwa KATIBA, SHERIA,  MATAMKO, NA MIKATABA mbalimbali ya kimataifa na kitaifa imetungwa ili itekerezwe na sio uvunjwe iweje leo serikali iliyosimamia na kuridhia mkataba huu inakuwa ya kwanza kuvunja mkataba huu? Sasa nini cha kufanya ili mkataba huu ili mateso,  manyanyaso ya namna kama hii ya wenye ulemavu kupigwa na kuteswa ikiwa ni pamoja na kusurubiwa ndani ya nchi yao yanakoma.
Pia utekelezaji wa thati wa mkataba huu ikiwa ni pamoja na mrejesho wa namna ya taifa au nchi mwanachama alivyotekeleza makubaliano ya mkataba huu yalivyofanyika nchini kitu ambacho sidhani kama kimefanyika na wahusika ya wenye ulemavu wakapewa au wakaona namna ya utekelezwaji ulivyofanikiwa.

Pia nawambea msamaha askari waliofanya kosa lile la kuwapiga wenye ulemavu kwa sababu naamini walikuwa hawajuwi mkataba huu unavyowataka kuwafanyia wenye ulemavu lakini niwatake asikali police na taasisi zingine mfatilie na kusoma mkataba huu ili yasijirudia kama yalivyotokea.  Asante kufatilia.

Source: correctnewstz.blogspot.com

Read more »

Wednesday, July 6, 2016

Olympic and Paralympic medallists share memories in ITF Olympic Book

The International Tennis Federation (ITF) today announced the publication of its official Olympic Book for Rio 2016: My Life, My Medal. One hundred and eighteen Olympic and Paralympic tennis medallists took part in the project to help promote the Rio 2016 Olympic and Paralympic Tennis Events.

Tennis returned as a full-medal sport at the Olympic Games at Seoul 1988, with the first Paralympic Tennis Event held at Barcelona 1992. The 224-page publication takes a look at the medallists from Seoul through London 2012, who share their stories of how the Olympics and Paralympics affected their lives. The book also shows the Olympians as they are today with original photography by 36 international photographers.

The book opens with all-time great Stefanie Graf, of Germany, who won singles gold at Seoul 1988 to crown a memorable year that saw her achieve the Grand Slam. She is joined by some of the game’s biggest stars of the last 30 years, including Andre Agassi (USA), Boris Becker (GER), Lindsay Davenport (USA), Novak Djokovic (SRB), Roger Federer (SUI), Justine Henin (BEL), Andy Murray (GBR), Rafael Nadal (ESP), Arantxa Sanchez Vicario (ESP), Monica Seles (USA), and Serena and Venus Williams (USA). Four-time singles gold medallist Esther Vergeer (NED), Shingo Kunieda (JPN), Peter Norfolk (GBR) and founder of wheelchair tennis Brad Parks (USA) are among the featured Paralympians.

ITF President David Haggerty said: “My Life, My Medal was inspired by American Tim Mayotte, who won a silver medal in Seoul, and who lists ‘Olympic medallist’ as his top achievement on his Twitter page 28 years later. This made us want to know how other tennis Olympians and Paralympians viewed theiachievement. This book allows you to read in their own words how important the Olympics have been, and continue to be, in their lives.”

Haggerty added: “Tennis’s return to the Olympics was an important milestone in the history of our sport. The Olympic effect has seen the number of ITF member nations increase from 147 in 1988 to a record 211 nations today. This has increased the number of nations competing at the highest level by about 40 percent.”
My Life, My Medal follows in the footsteps of the highly successful ITF publications, Aspire, Inspire and Journey to Beijing, that were produced for the last two Olympic Tennis Events.

The 2016 Olympic Tennis Event will be held at the Olympic Tennis Centre in Barra Olympic Park on 6-14 August, while the 2016 Paralympic Tennis Event will be held at the same venue on 9-16 September.

A list of the players included in the book is below.
Photographs from the ITF Olympic Book are available to media. Please contact ITF Communications for detai
Featured Medallists (P = Paralympians)

Argentina: Juan Martin del Potro, Javier Frana, Christian Miniussi, Gabriela Sabatini, Paola Suarez, Patricia Tarabini

Australia: Nicole Bradtke, Daniela Di Toro (P), David Hall (P), Rachel McQuillan, Alicia Molik, Branka Pupovac (P), Elizabeth Smylie, Wendy Turnbull, Todd Woodbridge, Mark Woodforde

Belarus: Victoria Azarenka, Max Mirnyi, Natalia Zvereva

Belgium: Els Callens, Justine Henin, Dominique Monami

Bulgaria: Manuela MaleevaCanada: Sebastien Lareau, Daniel Nestor

Chile: Fernando Gonzalez, Nicolas Massu

China, PR: Li Ting, Sun Tian-Tian, Yan Zi, Zheng Jie

Croatia: Mario Ancic, Goran Ivanisevic, Ivan Ljubicic, Goran Prpic

Czech Republic: Andrea Hlavackova, Lucie Hradecka, Helena Sukova

France: Julien Benneteau, Arnaud di Pasquale, Richard Gasquet, Stephane Houdet (P), Michael Jeremiasz (P), Michael Llodra, Amelie Mauresmo, Jo-Wilfried Tsonga

Georgia: Leila Meskhi

Great Britain: Neil Broad, Tim Henman, Andy Murray, Laura Robson, Peter Norfolk (P)

India: Leander Paes

Israel: Noam Gershony (P)

Japan: Shingo Kunieda (P)

Netherlands: Kristie Boogert, Monique Kalkman (P), Miriam Oremans, Maaike Smit (P),
 Chantal Vandierendonck (P), Esther Vergeer (P)

Russia: Andrei Cherkasov, Elena Dementieva, Yevgeny Kafelnikov, Maria Kirilenko, Nadia Petrova, Dinara
 Safina, Vera Zvonareva

Serbia: Novak Djokovic

Slovakia: Miloslav Mecir

South Africa: Wayne Ferreira, Piet Norval

Spain: Jordi Arrese, Sergi Bruguera, Sergio Casal, Alex Corretja, Albert Costa, Anabel Medina Garrigues, Conchita Martinez, Rafael Nadal, Virginia Ruano Pascual, Emilio Sanchez, Arantxa Sanchez Vicario

Sweden: Simon Aspelin, Stefan Edberg, Anders Jarryd, Thomas Johansson

Switzerland: Roger Federer, Marc Rosset, Stan Wawrinka

USA: Andre Agassi, Bob Bryan, Mike Bryan, Lindsay Davenport, Gigi Fernandez, Mary Joe Fernandez, Ken Flach, Zina Garrison, Brad Gilbert, Tim Mayotte, Brad Parks (P), Lisa Raymond, Robert Seguso, Monica Seles, Pam Shriver, Nick Taylor (P), David Wagner (P), Serena Williams, Venus Williams

Read more »

Thursday, April 28, 2016

Ukawa wawakaanga Ridhwan, Mama Salma

HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam imewakaanga wanaotajwa kumiliki Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA) bila kufuata utaratibu, anaandika Pendo Omary.

Hatua hiyo imekuja baada ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inayoongozwa Ukawa kuzuia Sh. 5 bilioni, fedha mali ya Kampuni ya Simon Group Limited.


Mama Salma Kikwete, Mke wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete na Ridhwan Kikwete, mtoto wa rais huyo na Prof. Juma Kapuya, aliyekuwa Mbunge wa Urambo Magharibi wanatajwa kuwa miongoni mwa wana hisa kwenye shirika hilo.

Simon Group Limited ililipa fedha hizo kwa halmashauri hiyo ikiwa ni sehemu ya malipo ya ununuzi wa hisa za UDA.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Saed Kubenea, Mbunge wa Jimbo la Ubungo amesema halmashauri haikuuza UDA licha ya Simon Group Limited kudai kununua.

Kwenye mkutano huo ambao pia uliohudhuriwa naIsaya Mwita Charles, Meya wa Jiji la Dar es Salaam Kubenea amesema, mkutano uliokabidha UDA kwa Simon Group uliitishwa bila baraka za wenye mali – Baraza la Madiwani la Jiji na Msajili wa Hazina na kwamba, ulihudhuriwa na watu wanne tu.

“Kwanza tunataka mtambue halmashauri haikuuza UDA kwa kuwa, Simon Group Limited wametumia hati ya UDA – mali ya wananchi kufanya biashara. Haturudishi fedha hizi mpaka tufanye hesabu, tujue kampuni hii imepata faida kiasi gani.

“Hata katika mradi wenyewe wa UDA-TR, kumesheheni utapeli. Unaoitwa mkutano mkuu maalum wa wana-hisa wa tarehe 10 Juni 2011, uliosimamiwa na Didas Masaburi, aliyekuwa Meya wa Jiji kuidhinisha pamoja na mengine, uuzaji wa hisa za UDA, haukuwa halali,” amesema Kubenea.

Kubenea amesema, mkutano uliokabidha UDA kwa Simon Group uliitishwa bila baraka za wenye mali – Baraza la Madiwani la Jiji na Msajili wa Hazina na kwamba, ulihudhuriwa na watu wanne tu

“Watu hawa ni Dk. Didas Masaburi mwenyewe ambaye alikuwa mwenyekiti; Mkurugenzi wa Simon Group, Robert Kisena ambaye alikuwa katibu; Mwanasheria wa jiji, Isaac Nassor Tasinga na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Phillip Mwakyusa,” amesema Kubenea.

Amesema, kwenye mkutano huo Masaburi alitangaza Kampuni ya Simon kuwa ‘imetimiza masharti yote ya mkataba wa kupewa hisa, mali na uendeshaji wa UDA.’

Ameeleza kuwa, mwaka 1983, Msajili wa Hazina alitoa asilimia 51 ya hisa na kuipa Halmashauri ya Jiji huku Serikali Kuu ikibakiwa na asilimia 49 na kwamba, shirika hili liliwekwa katika orodha ya mashirika ya kurekebishwa na serikali mwaka 1997.

“Taarifa ya serikali ya tarehe 3 Agosti 2011 kwenda Kamati ya Bunge ya Miundombinu inaeleza mkutano huo ulikuwa batili kwa kuwa, ulikiuka Katiba ya UDA, kifungu namba 45 kutokana na kutotimia kwa akidi na kukosekana kwa msajili wa hazina,” amesema Kubenea.

Taarifa hiyo imeeleza, kikao hicho hakikuwa na mamlaka ya kufanya uamuzi, na kuwa maazimio yote yaliyofikiwa yalikuwa batili.

“Kwa taarifa hii pekee, serikali ilipaswa kuiondoa Simon Group kwenye uendeshaji wa UDA ikiwemo kukodishwa mali zake, hadi hapo uchunguzi wa suala hilo utakapokamilika. Haikufanya hivyo,” amesema Kubenea.

Kubenea amesema, kwa taarifa hiyo pekee ilitosha serikali kuchunguza na kuwachukulia hatua wote waliohusika, hasa kwa kuzingatia kuwa, kabla ya kikao hicho, tayari Masaburi alishapokea barua ya tarehe 28 Februari 2011 kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu iliyomuagiza kusitisha mara moja mchakato wa kuuza hisa za serikali ambazo hazijagawiwa.

Akinukuu barua kutoka kwa Waziri Mkuu yenye Kumbukumbo Na. 185/295/01/27, amesema Masaburi na wenzake waliendesha mkutano huo wakiwa na kabrasha la Katiba ya UDA ambayo vipengele vyake vilikuwa vinakataza walichokifanya.

“Kipengele cha 2.0 cha mkataba kinaeleza mauzo ya hisa 7,880,303 ambazo hazijagawanywa ambapo kwa majibu wa kipengele cha 2.2, mnunuzi alipaswa kulipa kwa awamu kiasi cha Sh. 1.1 bilioni,” amesema.

Aidha, anasema malipo ya kwanza ya Sh. 285. 6 milioni sawa na asilimia 25 ya malipo yalipaswa kufanywa katika kipindi cha siku zisizozidi 14 tangu mkataba kufungwa.

Lakini Simon Group haikulipa kiasi kamili kwa mujibu wa mkataba na hata kiasi ilichotoa ilikilipa nje ya siku zilizotajwa na mkataba.

Read more »

Tuesday, March 1, 2016

BEI MPYA YA MAFUTA KIANZA KUTUMIKA KESHO TAREHE 2/3/2016

Read more »

Sunday, February 21, 2016

TUME YA UCHAGUZI YAKANUSHA UZUSHI ULIOENEA KUWA VYAMA VYA SIASA HAVIJAPEWA RUZUKU ZAO.

Read more »

Friday, February 19, 2016

Today Jacqueline Mengi and Faraja Nyalandu Gave Us Corporate Chic Look Goals .

Faraja Nyalandu visited Jacqueline Mengi at her office and this is what they wore .

Faraja is wearing all white suit and Black pumps while Jacqueline is dressing up in a floral dress that went perfect with her Yellow shoes .

Read more »

Thursday, February 18, 2016

AFUKUZWA CCM AKIDAIWA KUMFANYIA KAMPENI LOWASA.

Geita. Halmashauri ya CCM Mkoa wa Geita imemvua ujumbe wa Mkutano Mkuu, Peter Mwininga baada ya kudaiwa kukiuka maadili ya Umoja wa Vijana (UVCCM).

Licha ya kukiuka maadili ya umoja huo, Mwininga anadaiwa kukisaliti chama hicho wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita kwa kuwatukana viongozi wa ngazi za juu kwa njia ya mtandao.

Akizungumza baada ya kikao hicho juzi, Katibu wa Siasa na Uenezi CCM mkoani hapa, Said Kalidushi alisema baada ya wajumbe wa halmashauri kuu kupokea malalamiko na mapendekezo kutoka UVCCM, waliamua kumvua nafasi ya ujumbe huo kutokana na kupungukiwa na sifa.

Kalidushi alisema wakati wa kampeni Mwininga alikihujumu chama chao na kumfanyia kampeni mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa, huku akijua wazi kuwa ni kosa.

Katibu wa UVCCM mkoani hapa, Mashaka Mshola alisema kitendo cha Mwininga kuvuliwa nafasi aliyokuwa nayo kinatokana na usaliti na huo ni mwanzo wa chama hicho kuwafukuza wasaliti

Read more »

Wednesday, February 17, 2016

SERIKALI YAAGIZA VYOMBO VYA HABALI KUZINGATIA SHERIA ZA WATU WENYE ULEMAVU

 Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Dkt Abdallah Possi akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(HawapoPichani) kuhusu vyombo vya habari kutekeleza Sheria ya Watu wenye Ulemavu katika kupata habari.

Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Dkt Abdallah Possi (Aliyekaa) akizungumza na baadhi ya waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kwa kikao chake na vyombo vya habari leo ofisini kwake Jijini  Dar es Salaam.

Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (WatuwenyeUlemavu) Dkt  Abdallah Possi ameviagiza vyombo vya habari nchini kuzingatia Sheria ya Watu wenye ulemavu kwa kuhabarisha kwa kuzingatia mahitaji ya watu wenye ulemavu katika kutoa habari,

Akitoa agizo hilo mbele ya vyombo vya habari leo Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam Waziri Possi amesema vyombo vya habari vinatakiwa kuwakumbuka na watu wenye ulemavu katika utoaji wa taarifa mbalimbali katika Magazeti, Radio naTelevisheni hasa kwa kuzingatia lugha za alama ambazo zitawawezesha kuelewa habari husika.

“ Naomba tubadilike wanahabari kwa kuwajali watu wenye ulemavu kwa kuwahabarisha na wao pia, nawataka wamiliki wa vyombo vya habari hususan Televisheni kuweka lugha za alama kwa ajili ya watu wenye ulemavu ili kuwawezesha kupata habari mbalimbali zinazojiri katika taifa”

“Vyombo vya habari vinatakiwa kubadili uono wao juu ya walemavu na sio kwa kuangalia mambo hasi tu yahusiyo walemavu kwamba wana shinda,hawawezi, wanahitaji msaada ila pia kwakuangalia mafanikio yao katika kuleta maendeleo ya taifa kiujumla” Alisema Dkt Possi.

Aidha Dkt Abdallah Possi amewataka waandishi wa habari hasa wa magazeti kuzingatia lugha wanazotumia  kandika habari za watu wenye ulemavu ili kuondoa fikra na dhana hasi na unyayapaa juu ya walemavu huku akitolea mfano baadhi ya lugha zinazotumika na baadhi ya waandishi katika kuandika habari zinazohusu watu wenye ulemavu kuwa hazistahili.

Ametaja mfano wa lugha ambazo sio sahihi katika uandishi wa habari za wenye ulemavu mfano maneno vipofu, viziwi,vilema na maneno mengine bali wanatakiwa kutumia maneno yenye staa na yasiyoleta picha ya unyanyapaa na udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu ili kuondokana na dhana ya unyanyapaa na udhalilishaji wa watu wenye ulemavu.

Kupata habari ni haki ya kila mtu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria No 9 ya Mwaka 2010 inavitaka vyombo vya habari kuhabarisha watu bila kuwabagua watu wenye ulemavu, tuelewe kwamba pia watu wenye ulemavu wana haki ya kupata taarifa kama watu wengine.

Read more »

Bodi ya Wazee Wa Chama Cha NRA Yasema Itashiriki Marudio Ya Uchaguzi Zanzibar

Chama cha National Reconstruction Allience NRA kimewataka wanachama na wananchi kwa jumla kupuuza tamko la aliyekuwa mgombea wa Chama hicho kwa nafasi ya Urais, Seif Ally Idd kuwa yeye na chama wamejitoa katika marudio ya Uchaguzi wa Zanzibar unaotarajiwa kufanyika Machi 20, mwaka huu.

Kwa mujibu wa Baraza la Wazee, Bodi ya chama na Kamati kuu ya Chama cha NRA msimamo wa kushiriki uchaguzi wa Zanzibar upo paleplae kama kikao cha kamati kuu cha Februari 6 mwaka huu kilivyoazimia.

Jijini Dar Es Salaam, Baraza la wazee na Kamati Kuu ya Chama cha NRA, Kimesema chama kitaendelea kushiriki uchaguzi kama kilivyodhamiria na kuwataka wanachama kushiriki uchaguzi huo kwa amani.

NRA Kimesema iwapo mgombea wa chama hicho Zanzibar amejitoa katika uchaguzi huo basi afuatae taratibu za kisheria kama alivyofuata taratibu za kugombea nafasi hiyo ya urais na sheria za chama.

Chama cha NRA kimesema katika nchi yoyote yenye Demokrasia, Uchaguzi ndiyo njia pekee ya kushika dola, NA kuwataka wananchi wa Zanzibar kushiriki kikamilifu katika uchaguzi huo.

Chama cha NRA ni miongoni mwa vyama 14 vilivyosimamisha wagombea Urais katika uchaguzi wa Octoba 25, 2015, baadaye kufutwa kutokana na kasoro mbalimbali na ambao unatarajiwa kurudiwa tena Machi 20 mwaka huu.

Read more »

TUNDU LISSU AHOJIWA NA POLISI KWA MDA WA SAA MOJA.

TUNDU LISSU NAYE AITWA POLISI KWA MAHOJIANO AHOJIWA KWA SAA MOJA

TUNDU Lissu, Mwanasheria wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) pia Mbunge wa Singida Magharibi leo jijini Dar es Salaam amehojiwa na Jeshi la Polisi kuhusu hoja alizozitoa kwenye Gazeti la MAWIO.

Lissu amehojiwa kwa zaidi ya saa moja Makao Makuu ya Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam baada ya kuhitajika kutoa maelezo kwa madai ya kutoa kauli za uchoelezwa zilizoandikwa kwenye Gazeti la MAWIO zilizohusu mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibar.

Habari iliyoandikwa na gazeti hilo iliyobeba kichwa cha habari ‘Machafuko yaja Zanzibar’ inaelezwa kuwa sababu ya serikali kulifungia gazeti hilo tarehe 15 Januari mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kutoa maelezo Lissu amesema, serikali inajaribu kumziba mdomo asizungumzie kuhusu suluhu ya mgogoro wa kisiasa unaoendelea visiwani Zanzibar wakati wahusika hawazingatii misingi ya demokrasia.

“Wale waliobebwa kwenye uchaguzi leo wanataka kutufumba midomo tusizungumzie masula ya uchaguzi wa Zanzibar kwani machafuko yanaweza kutokea visiwani humo kwa tahadhari hiyo wanatuita wachochezi,” amesema Lissu.

Amesema kuwa, wao wametoa tahadhari ili yasitokee machafuko na umwagikaji wa damu na kwamba, Rais John Magufuli atawajibika kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) kama alivyowajibishwa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.

Amesema, mahojiano yake na Gazeti la Mawio ndio yaliyosababisha yeye kuitwa na kuhojiwa na polisi na kwamba, mtazamo wake ulioandikwa kwenye gazeti hilo ndio umechangia kufutwa kwa gazeti hilo.

Amesema kuwa hatokubali kuzibwa mdomo hata kama watatumia nguvu ya polisi.

Amesema, hatua ya Rais Magufuli kukakataa kujihusisha na mgogoro wa Zanzibar haikubaliki kwa kuwa ndiye ndiye atakayepeleka jeshi pale vurugu zitakapotokea.

Lissu amefika polisi hapo akiwa na mawakili wa watatu wa Chadema ambao ni Peter Kibatala, Fedrick Kiwelo na Hekima Mwasibu.

Amesema, baada ya mahojiano hayo polisi watapeleka jalada lake kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kwa hatua zaidi.

Read more »

MHINDI AFUKUZWA KAZI KWA KUWAITA WAFANYAKZI MANYANI

Raia wa India, Dennis Smith ameachishwa kazi katika Hoteli ya Ramada kwa madai ya kuwatukana wafanyakazi wa ngazi za chini akiwaita nyani.

Smith, ambaye ni meneja wa chakula na vinywaji wa hoteli hiyo, aliwatukana na kuwadhalilisha wafanyakazi hao siku ya Sikukuu ya Wapendanao akiwatuhumu kushindwa kuandaa meza vizuri.

Kutokana na udhalilishaji huo, wafanyakazi wa hoteli hiyo jana waligoma wakishinikiza meneja huyo asimamishwe kazi au wao waache kazi.

Wakizungumza jana, baadhi ya wafanyakazi ambao waliomba majina yao yahifadhiwe walisema tabia ya meneja huyo imekuwa sugu na tukio la juzi lilikuwa halivumiliki. Walisema raia huyo wa India amekuwa mwenye majivuno na kutoa lugha chafu dhidi yao.

“Tumechoshwa, anatuitaje sisi nyani, hii tabia ni ya muda mrefu na sasa hatuwezi kuivumilia,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.

Mwakilishi wa wafanyakazi hao, Mathew Misalaba alisema bosi huyo amekuwa akiwarushia maneno ya kuwadhalilisha kila wanapofanya makosa hata kidogo.

Alisema licha ya uongozi wa hoteli kuahidi kumsimamisha kazi Smith, wamelipeleka suala hilo polisi ili hatua stahiki zichukuliwe.

Meneja Rasilimaliwatu wa hoteli hiyo, Sebastian Nchimbi alisema tayari Smith ameachishwa kazi kutokana na tukio hilo.

“Tulizungumza na wafanyakazi wakatuambia kuwa hawataki Smith awepo kazini na sisi tukafanya uamuzi ili kuwalinda wafanyakazi wetu,” alisema.

Alisema waliamua kumwachisha kazi Smith baada ya kupata malalamiko mengi kutoka kwa wafanyakazi hao.

“Si tukio la mara ya kwanza na ndiyo maana tulipoona yamezidi tuliamua kuchukua hatua,” alisema.

Hata hivyo, Nchimbi alimsifu Smith akisema ni mtendaji mzuri na alikuwa na tija kwa hoteli hiyo ya kitalii lakini hakuwa na kauli nzuri kwa wafanyakazi Waafrika.

“Kiutendaji ni mzuri mno… yaani kwetu sisi tunapoteza mtu hasa, tatizo ni mdomo tu,” alisema.

Read more »

Friday, January 29, 2016

Mbwana Aly Samatta eindelijk in Genk.

Mbwana Aly Samatta (° Dar es Salam 23 december 1992, 1.80 m en 75 kg) is een tweevoetige centrumspits die ook als rechtsbuiten kan uitgespeeld worden. Hij komt over van het Congolese TP Mazembe.

Met deze club won hij in 2015 de Afrikaanse Champions League, werd hij vier keer op rij Congolees kampioen en won hij twee keer de Supercup.

Samatta werd intussen eenentwintig keer geselecteerd voor de nationale ploeg van zijn vaderland Tanzania.

In die wedstrijden scoorde hij zeven doelpunten.

In 2015 werd hij uitgeroepen tot beste Afrikaanse voetballer spelend op het Afrikaanse continent. Hij tekende een contract tot op het einde van het seizoen 2019 - 2020.

Straks krijgen jullie een verslag van de voorstelling en een eerste gesprek met Samatta.

Read more »

Wednesday, January 6, 2016

IBRAHIM AJIB: IS TREASURE FOR THE NATIONAL TEAM OF TANZANIA

Among the things that we devote our attention is Kismet and praise for all that is good for all Canadian Department, to the games starting last year we have to follow through to close Very young player, it's not another IBRAHIM  Ajib.

since last year Ajib dreams of scoring three in the same game in the 42nd minute came to pass after the first period scoring three successful and convincing leave with the ball.

That's been a hat-trick of three to Ajib at Simba but is second to him in the Vodacom Premier League.

Ajib scored a hat-trick in his first Cup championship Zanzibar Revolution then blew another hat-trick in the Premier League last season and taking other third goal in the Premier League this season against MajiMaji
Hat-trick it is the second on Vodacom Premier League this season after scoring a hat-trick Kiiza first this season when Lion when against Kagera Sugar at the national stadium.

Read more »

Monday, January 4, 2016

NATOA HOJA : WANAMICHEZO TUJITATHMINI MWAKA 2016 UMEANZA

Kama ilivyo miaka yote, Tanzania imekuwa ikivurunda katika michezo huku vikitolewa visingizio vya kila aina.

Mwaka wa 2015, kimsingi ndiyo umemalizika na ninaweza kusema hakukuwa na mafanikio katika michezo kwa ujumla wake.

Tanzania ilikuwa ikisifika katika fani mbalimbali za michezo, lakini kadri miaka inavyokwenda, imekuwa ikipoteza mwelekeo wake na hata kutia aibu.

Wanamichezo wetu walionyesha hawawezi, wameonyesha bado hawajakomaa mbele ya wanamichezo wa mataifa wenzao ya Afrika na dunia.

Hakika mwaka 2015 ulikuwa wa aibu katika michezo. Tulishindwa kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali hata ya Kanda za Tano, Kanda ya Sita kwa mpira wa kikapu, mikono michuano mbalimbali na mingine mingi ambayo tumeandaa sisi wenyewe.


Inasikitisha kwa kweli kuwa Tanzania imefutika katika ramani ya michezo na kuna kila sababu kuona mwaka huu inarudi upya kabisa.

Ifike hatua kuwe na mfululizo wa kumkabidhi Rais vikombe kwa vijana wake kuwa walichokifanya ndicho hiki.

Hebu, tujiulize, mwaka jana tumemkabidhi Rais vikombe vingapi kuwa vijana wetu wamefanya kazi nzuri nje na ndani ya nchi zaidi ya Azam na Kombe la Cecafa?


Tujiulize, tumemkabidhi medali ngapi Rais kuwa vijana wake wamepigana nje ya nchi na wakaleta heshima? Ni aibu, halafu eti Waziri mwenye dhamana ya michezo, anajisifu kuwa eneo la michezo limepiga hatua?


Kwa mwaka 2016, kuna haja ya kuwa na uwajibikaji wa jumla, vyama vya michezo, Baraza la Michezo la Taifa, BMT, Kurugenzi ya Michezo, wizara kwa ujumla wake kuwa karibu na utendaji wa vyama vya michezo na wadau wa michezo kuona hatua nyingine mpya za mwaka huu.

Nimekuwa nikiandika, hivi BMT wanafanya nini? Hivi na wao watajigamba wanasimamia michezo wakati iko katika hali mbaya? Kurugenzi ya Michezo nayo itasema wanasimamia michezo Tanzania ikiwa katika hali hiyo?


Ni kukumbushana na ninaamini BMT ina kalenda za vyama vyote vya michezo ya mwaka mzima, hivyo ni wajibu wake kuvikumbusha ama kufuatilia kwa karibu maandalizi yake tena kuanzia Januari hii.

Kusiwe na visingizio tena, kwamba kila mmoja anatakiwa kufanya kile anachostahili kufanya ili Tanzania kupiga hatua za mbali katika michezo.

Mafanikio ama kufanya vizuri kwa vyama vya michezo, kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuleta matumaini ya kufanya vizuri katika michezo kimataifa, lakini kama viongozi wataendelea kupigwa ‘AC’ ofisini na viti vya matairi na kuzunguka, kamwe hakutakuwa na maendeleo, hilo liko wazi.

Kuendelea kukimbia pekupeku, mabondia kukosa maandalizi ya maana ni wazi hatuwezi kupata medali.

Hapa yanayofanyika ni masihara tu kwani hata hayo maandalizi ya Michezo ya Olimpiki mwaka huu huko Rio de Janeiro, Brazil maandalizi yake hayaeleweki.

Labda niseme, michezo imepata Waziri anayeweza kwenda na kasi ya sasa, Hapa Kazi tu na ifike hatua mwaka huu uwe wa mafanikio katika michezo kwa kuonyesha dira mpya, mwelekeo mpya na kila mwenye wajibu na majukumu katika michezo, afanye kazi kwa nafasi yake kwa wakati wake.

Ukweli wa Watanzania wanapenda michezo na wako tayari kulipa fedha nyingi kupata burudani, tatizo hao waliopewa dhamana kusimamia sekta ya michezo nchini, wamejaaliwa kwa ubabaishaji wa hali ya juu.

Read more »

Saturday, December 26, 2015

Louis van Gaal: Odds slashed on Manchester United sacking manager after Stoke defeat

Odds on Louis van Gaal being the next Premier League manager to be sacked have been slashed by various bookies - with one even deciding to pay out.

Manchester United suffered a terrible defeat at Stoke City and are now without a win in their last seven matches, their worst run of form since December 1989.

Van Gaal, who has been heavily criticised in recent weeks for the side's awful form and boring style of play, is the heavy favourite to be out of a job soon.

With Jose Mourinho also lurking after being sacked by Chelsea, the future is looking bleak for the Dutchman. Odds shortened on the Portuguese taking over from his former mentor, and is as short as 8/13.

Read more »

Thursday, December 10, 2015

TPC WALIVYO SIVYO WALIVYOKUWA HAPO ZAMANI

Tanzania Paralympic  yaanzisha rasimi mchezo wa sitting Volleyball kwa kufanya shindano kubwa sana lililofadhiliwa na taasisi ya AGTOS FOUNDATION, kwa kuanzisha huku mchezo huu ndio kusema sasa wameanza rasmi na kwa kasi ya ajabu sana kwenye michezo ya walemavu kwa nchi  ya Tanzania.
 Wakizungumza na mwandisha wa blog yetu , wachezaji wa mchezo huu na michezo mingie wheelchair baskatball walisema, " kwaakeli tumeflahi sana kwa jitihada kubwa zilizofanywa na Uongozi mpya wa TNPC kwa kuanzisha shindano kama hili lenye lengo la kuhamasisha michezo ya watu wenyer ulemavu na tuna waomba waendelee hivihivi kwa michezo ni ajira  kwa watu kama sisi tusiokuwa na ajila" alinukuliwa  mchezaji STEVEN MANUMBU.
Pia akizungumza katibu wa TNPC amabae na ni mchezaji bwana Peter Sarungi alisema, "tunasukuru sana vyombo vya habari kwa sapoti yenu , tunawashukuru sana AGTOS FOUNDATION kwa sapoti yao kwentu ukizingatia ni mara ya kwanza kuomba pesa kwao na tumepa kutokana na maombi yetu kuwafulahisha sana na kuwauma kutusaidia kiasi cha pesa"
Read more »

Wednesday, December 9, 2015

TOKYO 2020 COMPETITION ATTRACTS THOUSANDS OF ENTRIES.

The open competition for the design of the Tokyo 2020 Olympic and Paralympic Games Emblems wrapped up successfully on Monday (7 December) with 14,599 entries.

Over the two-week period of the contest, Tokyo 2020 received 12,900 individual entries and 1,699 group entries.

“We were delighted to receive such a huge number of applications and that so many people actively took part in the competition. I firmly believe the
great passion shown by all applicants will serve to further drive the success of the Tokyo 2020 Games. It will be an extremely difficult task to select a single winning entry from among so many, but we will ensure that our selection process is fair, transparent and meets with general approval.

I would like to thank everyone who worked so hard on their designs and made the competition such a great success,” said Ryohei Miyata, Chairperson of the Tokyo 2020 Emblems Selection Committee.


The next stage of the selection process will consist of three steps:
- The organising committee will begin checking that submitted entries comply with format and design requirements with immediate effect.

- From Tuesday, 15 December, valid entries will be reviewed by the Tokyo 2020 Emblems Selection Committee and a group of 20 additional professional designers. Entries will be evaluated for quality of design, and a first round of selection will be conducted to select between 100–200 shortlisted entries.
- From Thursday, 7 January, the Tokyo 2020 Emblems Selection Committee will re-evaluate selected designs and narrow them down to a final shortlist of 3 or 4 designs.

The Tokyo 2020 Emblems will be announced in spring 2016.
The winning entry will receive an official invitation to attend the opening ceremonies of both the Tokyo 2020 Olympic and Paralympic Games.

The competition was open to everyone regardless of previous experience or formal qualifications, and welcomed both individual and group applications. Individual competition entries were invited from Japanese nationals over 18 years-old and foreign nationals over 18 years-old with the right of residence in Japan.

Children and foreigners not resident in Japan were also able to take part via the group entry system (10 persons maximum) as long as at least one person met the above age, nationality and residential requirements.
Read more »

Thursday, December 3, 2015

MAMBO AMBAYO YALIVUMA NA KUFRAHISHA WENGI KABLA YA SIKU YA WATU WENYE ULEMAVU DUNIANI DESEMBA 3/ 2015

  Nianze kwa kunukuu maneno ya kijana mwenye ulemavu na jasiri ambae kiukweli nimwite asiepende kucheza mbali na furusa pindi zinapompitia karibu nae ni aliekuwa mgombea uspika wa bunge la jamhuli ya muungano wa tanzania Bwana Peter Sarungi.


"Ndugu jamaa marafiki na wadau wangu wote na popote walipo, nitoe shukrani zangu za dhati kwa sappoti yenu toka nilivyoanza hatua ya kwenda kuwa spika wa bunge.



Ki ukweli nimefarijika sana na mapenzi yenu makubwa kwangu na kunichangia kwa hali na mali pamoja na ushauri mliokuwa mkinipa na kunifariji. 

Nilikwenda kushindana lakini pia nilikwenda kuzindua hatua zangu nyingi za mbele katika siasa.   
Nashukuru malengo yangu yamefanikiwa kwa 90% na huu ni ushindi kwangu kwa kuweza kufanikisha sauti yangu ya siasa kusikika kwa nchi nzima na kwa watawala wa nchi kwa mara ya kwanza."

Mimi nikiwa kama mtu mwenye ulemavu napenda sana kumpongeza bwana Sarungi kwa ujasili wa kutuwakirihsa vizuri watu wenye ulemavu na kutuondolea unyanyapa mabao ulikuwa bado umeganda kwenye baathi ya vichwa watanzania wakizani kuwa walemavu hawawawezi kumbe ndivyo sivyo, pia najuwa waliowengi wataungana nami bila kujali hali zetu za ulemavu kumpongeza Bwana sarungi.

Kwa kuzingatia maneno yako nndugu sarungi najuwa una malengo mengi sana ya kisiasa kama nilivyokunukuu napenda nimuombe mungu kwa niaba yako akupe moyo wa kujibidiisha katika kufikia malengo yako ambayo kiukweli yanafaida kwako na jamii nzima ya watu wenye ulemavu, kukosa uspika sio kukosa na mengine kaza buti na ukiwa unatambua kuwa mungu yupo pamoja na wewe kwa kila hatuwa. Amin




Read more »

Popular Posts

Author

Yohana Mwila

Translator

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
Copyright © 2013 CORRECT NEWSTZ BLOG. Powered by Blogger.
Blogger Template by Bloggertheme9
+255 (784) 033-443yohanamwila@gmail.com