Thursday, December 3, 2015

MAMBO AMBAYO YALIVUMA NA KUFRAHISHA WENGI KABLA YA SIKU YA WATU WENYE ULEMAVU DUNIANI DESEMBA 3/ 2015

Posted by Unknown  |  Tagged as:

  Nianze kwa kunukuu maneno ya kijana mwenye ulemavu na jasiri ambae kiukweli nimwite asiepende kucheza mbali na furusa pindi zinapompitia karibu nae ni aliekuwa mgombea uspika wa bunge la jamhuli ya muungano wa tanzania Bwana Peter Sarungi.


"Ndugu jamaa marafiki na wadau wangu wote na popote walipo, nitoe shukrani zangu za dhati kwa sappoti yenu toka nilivyoanza hatua ya kwenda kuwa spika wa bunge.



Ki ukweli nimefarijika sana na mapenzi yenu makubwa kwangu na kunichangia kwa hali na mali pamoja na ushauri mliokuwa mkinipa na kunifariji. 

Nilikwenda kushindana lakini pia nilikwenda kuzindua hatua zangu nyingi za mbele katika siasa.   
Nashukuru malengo yangu yamefanikiwa kwa 90% na huu ni ushindi kwangu kwa kuweza kufanikisha sauti yangu ya siasa kusikika kwa nchi nzima na kwa watawala wa nchi kwa mara ya kwanza."

Mimi nikiwa kama mtu mwenye ulemavu napenda sana kumpongeza bwana Sarungi kwa ujasili wa kutuwakirihsa vizuri watu wenye ulemavu na kutuondolea unyanyapa mabao ulikuwa bado umeganda kwenye baathi ya vichwa watanzania wakizani kuwa walemavu hawawawezi kumbe ndivyo sivyo, pia najuwa waliowengi wataungana nami bila kujali hali zetu za ulemavu kumpongeza Bwana sarungi.

Kwa kuzingatia maneno yako nndugu sarungi najuwa una malengo mengi sana ya kisiasa kama nilivyokunukuu napenda nimuombe mungu kwa niaba yako akupe moyo wa kujibidiisha katika kufikia malengo yako ambayo kiukweli yanafaida kwako na jamii nzima ya watu wenye ulemavu, kukosa uspika sio kukosa na mengine kaza buti na ukiwa unatambua kuwa mungu yupo pamoja na wewe kwa kila hatuwa. Amin




0 comments:

Popular Posts

Author

Yohana Mwila

Translator

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
Copyright © 2013 CORRECT NEWSTZ BLOG. Powered by Blogger.
Blogger Template by Bloggertheme9
+255 (784) 033-443yohanamwila@gmail.com