Monday, January 27, 2014

SALAMU ZA MWAKA MPYA TOKA KWANGU

Posted by Unknown  |  Tagged as:

Kwanza kabisa napenda niwatakie heli ya mwaka mpya wasomaji wa blog yangu kwani ni jambo la kumshukuru sana mungu kufika mwaka 2014 kwa najuwa hakuna hata mmoja miongoni mwetu ambae alitarajia au alijuwa kuwa atafika mwaka huu 2014 ila ni mungu kwa upenda wake kwetu, tumeuona, na hata kwa wale ambao hawajauona pia tuwaombee mungu awalaze mahali pema peponi Amina.

PONGEZI KWAO

kwa viongozi wote waliowajibika ama kwa kushindwa kazi au kwa kuwaachia wengine nao wafanye kazi walizokuwa wanafanya wao katika nafasi za uongozi wa serikali au wa vyama vya michezo .
Kwa viongozi wa serikali napenda sana kuwapongeza mawaziri walioamua kujihuthuru kwa hiali yao bila kuwajibishwa baada ya kuona mambo yanakwenda ndivyo sivyo katika wizara walizokuwa wanazitumikia,
Nawapongeza sana kwani wameonyesha kuwa wamekomaa kisiasa na pia wameonyesha kuwa wanaheshimu sana wananchi waliowachagua na pia wameonyesha wanauzalendo wa kutosha.



0 comments:

Popular Posts

Author

Yohana Mwila

Translator

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
Copyright © 2013 CORRECT NEWSTZ BLOG. Powered by Blogger.
Blogger Template by Bloggertheme9
+255 (784) 033-443yohanamwila@gmail.com