Monday, June 19, 2017

USEMAVYO MKATABA WA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU

Kutokana na tukio la majuzi la kupigwa na kiteswa kwa watu wenye ulemavu nchini Tanzania wakidaiwa kufanya maandamo,  wakidai yako yao ya msingi iliyomo kwenye mkataba wa kimataifa IBARA YA 27 KIPENGERE CHA (f) “Kuendeleza ajira binafsi, fursa za biashara, ushirika na kuanzisha biashara;” na hii ni mahususi kwa watu wenye ulemavu pamoja ibara na vingere vingine vingi kama nilivyoviolozesha hapa chini.
Pia katika mkataba huu ni kwamba haujaacha kitu kwani umetowa majukumu mazuri na makubwa ya kutekerezwa kwa kila idara ya wizara na taasisi zote nini wajibu wao juu ya watu wenye ukemavu ikiwemo jeshi la police,  kinachonisikitisha ni kwamba elimu haijafika kwa wahusika hususani jeshi ka police nduo maana hawazinmtambuwa haki za wenye ulemavu kwa mjibu wa mkataba huu.
Mimi kama mwanaharakati natamani sana kila mtu atambuwe namna mkataba huu unavyosema ila nashindwa kuelewa mamlaka zinazohusika kwanini mpaka leo kuna watu au taasisi ambazo dhahili zimeonyesha kutombua na kufahamu mkataba huu unavyowataka kuwatendea watu wenye ulemavu,  na yote hii ni kwa sababu mamlaka zinazohusika zimeshindwa kuufikisha na kusambaza elimu hii mhimu iliyosainiwa na serikali yetu chini ya MHE: RAIS DK JAKAYA MRISHO KIKWETE.  Mwaka 2009.

IBARA NA VIPENGERE VYA
MKATABA WA KIMATAIFA WA HAKI ZA WATU WENYE UKEMAVU.

IBARA YA 1-- MADHUMUNI
Maafikiano haya yameandaliwa ili kuhakikisha kwamba:Watu wenye ulemavu ni pamoja na watu wenye vilema vya kudumu (mathalani: viungo, akili n.k) na wale ambao kwa sababu mbalimbali
hawajumuishwi katika jamii (mfano kutokana na vizuizi vya kimtazamo,
lugha, mazingira na sheria).

IBARA YA 11-- HALI YA HATALI NA DHARULA.
kutokana na majanga Nchi zitahakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanalindwa wakati wa vita, majanga ya asili au
dharura nyinginezo.

IBARA YA 15 -- KUTOFANYIWA MATESO UKATILI AU KUDHALILISHWA.
1. Hakuna mtu atakayeteswa, kutendewa au kuadhibiwa katika hali ya kikatili au
kiudhalilishaji. Hakuna mtu atakayelazimishwa kushiriki katika majaribio ya kisayansi au kitabibu.

IBARA YA 16 -- KUTINYONYWA KUTOFANYIWA VURUGU AU KUNYANYASWA.
Nchi:
1. Zitapitisha sheria na kuchukua hatua
nyinginezo ili kuhakikisha kuwa watu wenye
ulemavu hawanyonywi au kudhalilishwa
wakiwa nyumbani au nje ya nyumbani.
2. Zitachukua hatua ya kuzuia udhalilishaji wa watu wenye ulemavu kwa kuwapa misaada na taarifa sahihi wao wenyewe
na familia zao.
3. Zitahakikisha kuwa sehemu na programu zinazowa-hudumia watu wenye ulemavu zinakaguliwa kila mara ili kudhibiti ukatili na manyanyaso

2. Nchi zinakubaliana,  kutunga sheria na kuchukua hatua nyingine ili kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu
wanalindwa dhidi ya mateso kama ilivyo kwa watu wengine.

IBARA YA 27 - KAZI NA AJIRA.
1. Watu wenye ulemavu wana haki ya kufanya kazi sawa na watu wengine;
wana haki ya kupata riziki kutokana na
kazi walizojiamulia kuzifanya katika
mazingira yaliyo wazi na yanayofikiwa na watu wote. Nchi zitatunga sheria na kuchukua hatua nyingi zinazofaa ili:
a) Kuondoa ubaguzi kwa misingi ya ulemavu katika maeneo yote ya ajira ikiwa ni
pamoja na katika hali ya kutafuta kazi, kuajiriwa kuendelea na ajira, kupandishwa cheo
kazini na kufanya kazi katika mazingira salama kiafya;
b) Kulinda ajira za watu wenye ulemavu kuhusu usawa katika malipo ya ujira kwa kazi
ile ile, usawa wa fursa, usalama kazini na uwezo wa kutoa malalamiko;
c) Kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanaweza kujiunga pamoja na kuingia
kwenye vyama vya wafanyakazi sawa na mtu mwingine yeyote;
d) Kuweka uwezekano wa watu wenye ulemavu kupata huduma za ushauri wa
mafunzo kazini.
e) Kupanua fursa za kazi, kuandishwa vyeo na kuwasaidia watu wenye ulemavu
kutafuta kazi na kudumu kazini;
f) Kuendeleza ajira binafsi, fursa za biashara, ushirika na kuanzisha biashara;
g) Kuajiri watu wenye ulemavu serikalini;
h) Kuhimiza na kuwasaidia waajiri kuajiri watu wenye ulemavu;
i) Kuwarahisishia watu wenye ulemavu kumudu kazi na mazingira yake kwa
kuhakikisha kuwa marekebisho yanafanyika kwa ajili yao;
j) Kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanapata uzoefu wa kazi katika soko la ajira;
k) Kukuza programu zinazowasaidia watu wenye ulemavu kurudi kazini na kudumu na
ajira zao.
2. Nchi zitahakikisha kuwa watu wenye ulemavu hawafanywi watumwa/watwana. Nchi zitawalinda dhidi ya ajira za kushurutishwa sawa na wanavyolindwa watu wengine.

Mwisho naomba nisisitize kuwa KATIBA, SHERIA,  MATAMKO, NA MIKATABA mbalimbali ya kimataifa na kitaifa imetungwa ili itekerezwe na sio uvunjwe iweje leo serikali iliyosimamia na kuridhia mkataba huu inakuwa ya kwanza kuvunja mkataba huu? Sasa nini cha kufanya ili mkataba huu ili mateso,  manyanyaso ya namna kama hii ya wenye ulemavu kupigwa na kuteswa ikiwa ni pamoja na kusurubiwa ndani ya nchi yao yanakoma.
Pia utekelezaji wa thati wa mkataba huu ikiwa ni pamoja na mrejesho wa namna ya taifa au nchi mwanachama alivyotekeleza makubaliano ya mkataba huu yalivyofanyika nchini kitu ambacho sidhani kama kimefanyika na wahusika ya wenye ulemavu wakapewa au wakaona namna ya utekelezwaji ulivyofanikiwa.

Pia nawambea msamaha askari waliofanya kosa lile la kuwapiga wenye ulemavu kwa sababu naamini walikuwa hawajuwi mkataba huu unavyowataka kuwafanyia wenye ulemavu lakini niwatake asikali police na taasisi zingine mfatilie na kusoma mkataba huu ili yasijirudia kama yalivyotokea.  Asante kufatilia.

Source: correctnewstz.blogspot.com

Read more »

Wednesday, July 6, 2016

Olympic and Paralympic medallists share memories in ITF Olympic Book

The International Tennis Federation (ITF) today announced the publication of its official Olympic Book for Rio 2016: My Life, My Medal. One hundred and eighteen Olympic and Paralympic tennis medallists took part in the project to help promote the Rio 2016 Olympic and Paralympic Tennis Events.

Tennis returned as a full-medal sport at the Olympic Games at Seoul 1988, with the first Paralympic Tennis Event held at Barcelona 1992. The 224-page publication takes a look at the medallists from Seoul through London 2012, who share their stories of how the Olympics and Paralympics affected their lives. The book also shows the Olympians as they are today with original photography by 36 international photographers.

The book opens with all-time great Stefanie Graf, of Germany, who won singles gold at Seoul 1988 to crown a memorable year that saw her achieve the Grand Slam. She is joined by some of the game’s biggest stars of the last 30 years, including Andre Agassi (USA), Boris Becker (GER), Lindsay Davenport (USA), Novak Djokovic (SRB), Roger Federer (SUI), Justine Henin (BEL), Andy Murray (GBR), Rafael Nadal (ESP), Arantxa Sanchez Vicario (ESP), Monica Seles (USA), and Serena and Venus Williams (USA). Four-time singles gold medallist Esther Vergeer (NED), Shingo Kunieda (JPN), Peter Norfolk (GBR) and founder of wheelchair tennis Brad Parks (USA) are among the featured Paralympians.

ITF President David Haggerty said: “My Life, My Medal was inspired by American Tim Mayotte, who won a silver medal in Seoul, and who lists ‘Olympic medallist’ as his top achievement on his Twitter page 28 years later. This made us want to know how other tennis Olympians and Paralympians viewed theiachievement. This book allows you to read in their own words how important the Olympics have been, and continue to be, in their lives.”

Haggerty added: “Tennis’s return to the Olympics was an important milestone in the history of our sport. The Olympic effect has seen the number of ITF member nations increase from 147 in 1988 to a record 211 nations today. This has increased the number of nations competing at the highest level by about 40 percent.”
My Life, My Medal follows in the footsteps of the highly successful ITF publications, Aspire, Inspire and Journey to Beijing, that were produced for the last two Olympic Tennis Events.

The 2016 Olympic Tennis Event will be held at the Olympic Tennis Centre in Barra Olympic Park on 6-14 August, while the 2016 Paralympic Tennis Event will be held at the same venue on 9-16 September.

A list of the players included in the book is below.
Photographs from the ITF Olympic Book are available to media. Please contact ITF Communications for detai
Featured Medallists (P = Paralympians)

Argentina: Juan Martin del Potro, Javier Frana, Christian Miniussi, Gabriela Sabatini, Paola Suarez, Patricia Tarabini

Australia: Nicole Bradtke, Daniela Di Toro (P), David Hall (P), Rachel McQuillan, Alicia Molik, Branka Pupovac (P), Elizabeth Smylie, Wendy Turnbull, Todd Woodbridge, Mark Woodforde

Belarus: Victoria Azarenka, Max Mirnyi, Natalia Zvereva

Belgium: Els Callens, Justine Henin, Dominique Monami

Bulgaria: Manuela MaleevaCanada: Sebastien Lareau, Daniel Nestor

Chile: Fernando Gonzalez, Nicolas Massu

China, PR: Li Ting, Sun Tian-Tian, Yan Zi, Zheng Jie

Croatia: Mario Ancic, Goran Ivanisevic, Ivan Ljubicic, Goran Prpic

Czech Republic: Andrea Hlavackova, Lucie Hradecka, Helena Sukova

France: Julien Benneteau, Arnaud di Pasquale, Richard Gasquet, Stephane Houdet (P), Michael Jeremiasz (P), Michael Llodra, Amelie Mauresmo, Jo-Wilfried Tsonga

Georgia: Leila Meskhi

Great Britain: Neil Broad, Tim Henman, Andy Murray, Laura Robson, Peter Norfolk (P)

India: Leander Paes

Israel: Noam Gershony (P)

Japan: Shingo Kunieda (P)

Netherlands: Kristie Boogert, Monique Kalkman (P), Miriam Oremans, Maaike Smit (P),
 Chantal Vandierendonck (P), Esther Vergeer (P)

Russia: Andrei Cherkasov, Elena Dementieva, Yevgeny Kafelnikov, Maria Kirilenko, Nadia Petrova, Dinara
 Safina, Vera Zvonareva

Serbia: Novak Djokovic

Slovakia: Miloslav Mecir

South Africa: Wayne Ferreira, Piet Norval

Spain: Jordi Arrese, Sergi Bruguera, Sergio Casal, Alex Corretja, Albert Costa, Anabel Medina Garrigues, Conchita Martinez, Rafael Nadal, Virginia Ruano Pascual, Emilio Sanchez, Arantxa Sanchez Vicario

Sweden: Simon Aspelin, Stefan Edberg, Anders Jarryd, Thomas Johansson

Switzerland: Roger Federer, Marc Rosset, Stan Wawrinka

USA: Andre Agassi, Bob Bryan, Mike Bryan, Lindsay Davenport, Gigi Fernandez, Mary Joe Fernandez, Ken Flach, Zina Garrison, Brad Gilbert, Tim Mayotte, Brad Parks (P), Lisa Raymond, Robert Seguso, Monica Seles, Pam Shriver, Nick Taylor (P), David Wagner (P), Serena Williams, Venus Williams

Read more »

Thursday, April 28, 2016

Ukawa wawakaanga Ridhwan, Mama Salma

HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam imewakaanga wanaotajwa kumiliki Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA) bila kufuata utaratibu, anaandika Pendo Omary.

Hatua hiyo imekuja baada ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inayoongozwa Ukawa kuzuia Sh. 5 bilioni, fedha mali ya Kampuni ya Simon Group Limited.


Mama Salma Kikwete, Mke wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete na Ridhwan Kikwete, mtoto wa rais huyo na Prof. Juma Kapuya, aliyekuwa Mbunge wa Urambo Magharibi wanatajwa kuwa miongoni mwa wana hisa kwenye shirika hilo.

Simon Group Limited ililipa fedha hizo kwa halmashauri hiyo ikiwa ni sehemu ya malipo ya ununuzi wa hisa za UDA.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Saed Kubenea, Mbunge wa Jimbo la Ubungo amesema halmashauri haikuuza UDA licha ya Simon Group Limited kudai kununua.

Kwenye mkutano huo ambao pia uliohudhuriwa naIsaya Mwita Charles, Meya wa Jiji la Dar es Salaam Kubenea amesema, mkutano uliokabidha UDA kwa Simon Group uliitishwa bila baraka za wenye mali – Baraza la Madiwani la Jiji na Msajili wa Hazina na kwamba, ulihudhuriwa na watu wanne tu.

“Kwanza tunataka mtambue halmashauri haikuuza UDA kwa kuwa, Simon Group Limited wametumia hati ya UDA – mali ya wananchi kufanya biashara. Haturudishi fedha hizi mpaka tufanye hesabu, tujue kampuni hii imepata faida kiasi gani.

“Hata katika mradi wenyewe wa UDA-TR, kumesheheni utapeli. Unaoitwa mkutano mkuu maalum wa wana-hisa wa tarehe 10 Juni 2011, uliosimamiwa na Didas Masaburi, aliyekuwa Meya wa Jiji kuidhinisha pamoja na mengine, uuzaji wa hisa za UDA, haukuwa halali,” amesema Kubenea.

Kubenea amesema, mkutano uliokabidha UDA kwa Simon Group uliitishwa bila baraka za wenye mali – Baraza la Madiwani la Jiji na Msajili wa Hazina na kwamba, ulihudhuriwa na watu wanne tu

“Watu hawa ni Dk. Didas Masaburi mwenyewe ambaye alikuwa mwenyekiti; Mkurugenzi wa Simon Group, Robert Kisena ambaye alikuwa katibu; Mwanasheria wa jiji, Isaac Nassor Tasinga na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Phillip Mwakyusa,” amesema Kubenea.

Amesema, kwenye mkutano huo Masaburi alitangaza Kampuni ya Simon kuwa ‘imetimiza masharti yote ya mkataba wa kupewa hisa, mali na uendeshaji wa UDA.’

Ameeleza kuwa, mwaka 1983, Msajili wa Hazina alitoa asilimia 51 ya hisa na kuipa Halmashauri ya Jiji huku Serikali Kuu ikibakiwa na asilimia 49 na kwamba, shirika hili liliwekwa katika orodha ya mashirika ya kurekebishwa na serikali mwaka 1997.

“Taarifa ya serikali ya tarehe 3 Agosti 2011 kwenda Kamati ya Bunge ya Miundombinu inaeleza mkutano huo ulikuwa batili kwa kuwa, ulikiuka Katiba ya UDA, kifungu namba 45 kutokana na kutotimia kwa akidi na kukosekana kwa msajili wa hazina,” amesema Kubenea.

Taarifa hiyo imeeleza, kikao hicho hakikuwa na mamlaka ya kufanya uamuzi, na kuwa maazimio yote yaliyofikiwa yalikuwa batili.

“Kwa taarifa hii pekee, serikali ilipaswa kuiondoa Simon Group kwenye uendeshaji wa UDA ikiwemo kukodishwa mali zake, hadi hapo uchunguzi wa suala hilo utakapokamilika. Haikufanya hivyo,” amesema Kubenea.

Kubenea amesema, kwa taarifa hiyo pekee ilitosha serikali kuchunguza na kuwachukulia hatua wote waliohusika, hasa kwa kuzingatia kuwa, kabla ya kikao hicho, tayari Masaburi alishapokea barua ya tarehe 28 Februari 2011 kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu iliyomuagiza kusitisha mara moja mchakato wa kuuza hisa za serikali ambazo hazijagawiwa.

Akinukuu barua kutoka kwa Waziri Mkuu yenye Kumbukumbo Na. 185/295/01/27, amesema Masaburi na wenzake waliendesha mkutano huo wakiwa na kabrasha la Katiba ya UDA ambayo vipengele vyake vilikuwa vinakataza walichokifanya.

“Kipengele cha 2.0 cha mkataba kinaeleza mauzo ya hisa 7,880,303 ambazo hazijagawanywa ambapo kwa majibu wa kipengele cha 2.2, mnunuzi alipaswa kulipa kwa awamu kiasi cha Sh. 1.1 bilioni,” amesema.

Aidha, anasema malipo ya kwanza ya Sh. 285. 6 milioni sawa na asilimia 25 ya malipo yalipaswa kufanywa katika kipindi cha siku zisizozidi 14 tangu mkataba kufungwa.

Lakini Simon Group haikulipa kiasi kamili kwa mujibu wa mkataba na hata kiasi ilichotoa ilikilipa nje ya siku zilizotajwa na mkataba.

Read more »

Tuesday, March 1, 2016

BEI MPYA YA MAFUTA KIANZA KUTUMIKA KESHO TAREHE 2/3/2016

Read more »

Sunday, February 21, 2016

TUME YA UCHAGUZI YAKANUSHA UZUSHI ULIOENEA KUWA VYAMA VYA SIASA HAVIJAPEWA RUZUKU ZAO.

Read more »

Friday, February 19, 2016

Today Jacqueline Mengi and Faraja Nyalandu Gave Us Corporate Chic Look Goals .

Faraja Nyalandu visited Jacqueline Mengi at her office and this is what they wore .

Faraja is wearing all white suit and Black pumps while Jacqueline is dressing up in a floral dress that went perfect with her Yellow shoes .

Read more »

Thursday, February 18, 2016

AFUKUZWA CCM AKIDAIWA KUMFANYIA KAMPENI LOWASA.

Geita. Halmashauri ya CCM Mkoa wa Geita imemvua ujumbe wa Mkutano Mkuu, Peter Mwininga baada ya kudaiwa kukiuka maadili ya Umoja wa Vijana (UVCCM).

Licha ya kukiuka maadili ya umoja huo, Mwininga anadaiwa kukisaliti chama hicho wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita kwa kuwatukana viongozi wa ngazi za juu kwa njia ya mtandao.

Akizungumza baada ya kikao hicho juzi, Katibu wa Siasa na Uenezi CCM mkoani hapa, Said Kalidushi alisema baada ya wajumbe wa halmashauri kuu kupokea malalamiko na mapendekezo kutoka UVCCM, waliamua kumvua nafasi ya ujumbe huo kutokana na kupungukiwa na sifa.

Kalidushi alisema wakati wa kampeni Mwininga alikihujumu chama chao na kumfanyia kampeni mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa, huku akijua wazi kuwa ni kosa.

Katibu wa UVCCM mkoani hapa, Mashaka Mshola alisema kitendo cha Mwininga kuvuliwa nafasi aliyokuwa nayo kinatokana na usaliti na huo ni mwanzo wa chama hicho kuwafukuza wasaliti

Read more »

Popular Posts

Author

Yohana Mwila

Translator

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
Copyright © 2013 CORRECT NEWSTZ BLOG. Powered by Blogger.
Blogger Template by Bloggertheme9
+255 (784) 033-443yohanamwila@gmail.com