Thursday, October 24, 2013

NI UJINGA KUSEMA TANZANIA NI KICHWA CHA MWENDAWAZI, WAKATI SIO KICHWA CHA MWENDAWAZIMU.ILA VIONGOZI WA TOC NA TPC NDIO WANASABABISHA TANZANIA IITWE KICHWA CHA MWENDAWAZIMU.

Posted by Unknown  |  Tagged as: ,



Kwanza naomba tutambuwe michezo sio mpira wa miguu tu! Bali ni michezo yote kama Riatha, Tennis, kurusha Tufe, kurusha Kisahani, Kuogelea, Mpira wa Magongo, Tebo Tennis, Ngumi, Netball, Handball, na michezo hii kwa nchi  nilizozita hushirikisha watu wenye walemavu na wasio na ulemavu, kwa kuwa lengo la taifa lolote lenye nia ya kulitangaza taifa lake na kutaka kupata medali kupitia michezo huwa halishuguliki na mpira wa miguu tu! Bali na michezo mingine.
Kwa mfano nchi za wenzetu kama Kenya, Uganda, Ethiopia, Rwanda, South Africa, na zinginezo hazifanyi vizuri sana kwenye mpira wa miguu, lakini kwenye michezo mingine mataifa yao yanajulikana sana Duniani kupitia michezo mingine ambayo sisi Tanzania hatutaki kuipa kipaumbele.
Jamaniwatanzania wenzangu kama soka imeshindikana tutowe furusa na kwenye michezo mingine sisi kama watanzania wenye uchungu na Taifa letu ambalo lina hamu sana ya siku moja tuanze kereta medali kama mvua na hatimae JINA la Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu Lisiwepo na lisije kuendelea kutajwa tena kwani ni aibu kwa taifa lenye vipaji rukuki sana vya wachezaji wa kila aina ya mchezo
Na  Siku zote nimekuwa nikisema ukweli na sitaweza kusifia kitu ambacho hakistahili sifa yoyote sioni sababu ya kusema safi kama sio safi sioni sababu ya kusema ndiyo kama jibu ni hapana siwezi sema one wakati ni ziro, Zaidi ya kucema kuwa serikali na watendaji wake tuanhane na mpira wa miguu unatuchelewesha kupata medali na kujulikana Duniani kwa  kuwa Tanzania ni nchi ina kila sababu ya kufikia zaidi ya walipo majirani zetu na wasio majirani zetu kwani tuna vipaji vya kila aina, nasema ni Ujinga kuendelea kufanya Biashara inayokutia hasara kila siku.
TFF mnayo majibu  juu ya kwanini soka letu halina radha , tukianza na ligi zetu bado hazijaonyesha sura ya kwamba siku moja timu yetu ya taifa itacheza soka lenye mvuto  ukitazama soka la leo pale taifa ni wazi kuwa  mchezo wa timu yetu umekuwa ni mchezo wa mchezaji mmoja mmoja sijaona soka la timu sijaona mchezo wa kitimu maana sijaona hata kama mabadiliko  yanayoweza kubadili mchezo nimeona wazi kukosekana kwa fulani mchezo wa timu nzima unabadilika.
Natoa ushauri kwa TOC na TPC na kama hamtasoma hapa basi nawaomba wanachama wa TOC ambao ni wajumbe  wa mkutano mkuu wakipata nafasi ya kuchangia katika mikutano yenu  naomba wanisemee yafuatayo ..
  1.  Ipo haja ya kuangalia upya jinsi gani ya mashindano yetu ya taifa ambayo ndio yanayoweza kuvumbua vipaji, waangalie jinsi mfumo unaotumika kuendesha mashindano haya mhimu, kama uendeshwaji wake unakizi viwango na vigezo.
  2. Maboresho katika usimamizi wa  Timu za Taifa za vijana zinapokuwa kambini na kwenye maandalizi ya aina yeyote kama hayana kaoro na kama yana kasoro basi kasoro hizo zirekebishwe bila kumwangalia mtu usoni, na bila kumwogopa mtu kwa aina yake awe savimbi, marehemu gadafi, marehemu hosama bini ladeni au kwa vyovyote atakavyokuwa kwa kuwatanzania au nafasi anayoishikiria hajajipa mwenyewe bali nyinyi wajumbe kwa kutuwakrisha watanzania tulio wengi ndio mmewapa.
  3. Kusuka upya timu za taifa ambazo zitatafutiwa michezo mingi ya kirafiki na ikiwezekana tukasimama kushiriki mashindano ya kimataifa hata kwa miaka miwili .
Na kwako msomaji unaweza ongezea mengine unayodhani yanafaa ili tusiendelee kuwa kichwa cha mwehu...
Ingia hapo TUMA MAONI ili uweze kuongezea ya kwako
 Captean:  yohana mwila.
                                                     www.yohanamwila.blogspot.com

0 comments:

Popular Posts

Author

Yohana Mwila

Translator

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
Copyright © 2013 CORRECT NEWSTZ BLOG. Powered by Blogger.
Blogger Template by Bloggertheme9
+255 (784) 033-443yohanamwila@gmail.com